info@hazinasaccos.co.tz +255 710 933 944
English | Swahili
Contact Us
emblem

HAZINA SACCOS

HAZINA SAVING AND CREDIT COOPERATIVE SOCIETY LTD
CHAMA CHA USHIRIKA WA AKIBA NA MIKOPO CHA HAZINA
hazina Logo
  • Kuhusu Sisi
    Historia Dira, Dhamira & Maadili Ukuaji
  • Uongozi
    Muundo Wajumbe wa Board Menegementi Kamati Ya Usimamizi Watendaji
  • Huduma Zetu
    Akiba Hisa Amana Mikopo Historia
  • Habari & Matukio
    Habari Matukio Video Maswali ya Wateja
  • Mifumo
    Portal Yetu Staff Mail
  • Nakala
  • Wasiliana Nasi
  1. Mikopo

Mikopo Yetu

Chagua mkopo unaokufaa na ujue masharti yake kwa urahisi.

1. Mkopo wa Tuliza Moyo

Kiwango cha mkopo huu ni kuanzia Tsh 300,000/= hadi Tsh.1,000,000 bila riba. Muda wa marejesho ni siku 30, mkopo huu hutolewa ndani ya masaa 24 baada ya kukamilisha taratiu za maombi.

2. Mkopo wa Dharura 1

Kiwango cha juu cha mkopo huu ni Tsh 5,000,000/= na kutoza riba 1.5% kwa mwezi. Muda wa juu wa marejesho ni miezi 12, mkopo huu hutolewa ndani ya masaa 24 baada ya kukamilisha taratibu za maombi.

3. Mkopo wa Dharura 2

Kiwango cha juu cha mkopo huu ni Tsh 10,000,000/= na kutoza riba 1.5% kwa mwezi. Muda wa juu wa marejesho ni miezi 24, mkopo huu hutolewa ndani ya siku saba (07) baada ya kukamilisha taratibu za maombi.

4. Mkopo wa Elimu

Kiwango cha juu cha mkopo huu ni Tsh 5,000,000/= na kutoza riba ya 0.42%. Muda wa kurejesha mkopo ni miezi 24. Fomu hupokelewa kuanzia tarehe 1 – 20 ya kila mwezi.

5. Mkopo wa Biashara

Kiwango cha juu cha mkopo huu ni mara tatu (3) ya akiba za mwanachama na kutoza riba ya 0.84% kwa mwezi. Muda wa kurejesha mkopo huu ni miezi 12 – 60. Fomu hupokelewa kuanzia tarehe 1-20 ya kila mwezi.

6. Mkopo wa Viwanja

Hutegemea na taratibu zitakazowekwa na chama kwa wakati huo.

7. Mkopo wa Mazishi

Kiwango cha juu cha mkopo huu ni 3,000,000/= na kutoza riba ya 0.42% . Muda wa kurejesha mkopo huu ni miezi 24 , mkopo huu hutolewa pale mwanachama anapokuwa amefiwa baba,mama, mtoto, mume au mke.

8. Mkopo wa sikukuuu

Kiwango cha juu cha mkopo huu ni 500,000/= na kutoza riba ya 0.84%. Muda wa juu wa kurejesha mkopo ni miezi 6. Hutolewa kwa sikukuu za Krismas, Pasaka, na Idd El-fitri

9. Mkopo wa Maendeleo

Kiwango cha juu cha mkopo huu ni mara tatu (3) ya akiba za mwanachama na kutoza riba ya 0.84%. Muda wa kurejesha mkopo huu ni miezi 12 – 60. Hutolewa mwishoni mwa mwezi na fomu hupokelewa kuanzia tarehe 1-20 ya kila mwezi.

10. Mkopo wa Ujenzi

Kiwango cha juu cha mkopo huu ni mara tatu (3) ya akiba za mwanachama na kutoza riba ya 0.84% kwa mwezi. Muda wa kurejesha mkopo huu ni miezi 12 – 60. Fomu hupokelewa kuanzia tarehe 1-20 ya kila mwezi.

11. Mkopo wa utaratibu wa Bank (Standing Order)

Kiwango cha juu ni Tsh 50,000,000.00 na kutoza riba ya 1.5%. Muda wa kurejesha ni miezi 48. Fomu hupokelewa kuanzia tarehe 1-20 ya kila mwezi.

Hazina Saccos

Chama cha ushirika wa akiba na mikopo kilichopo Tanzania, kinachotoa huduma za kifedha kwa wanachama wake ili kuwasaidia kujiimarisha kiuchumi.

Viungo Muhimu

  • Kuhusu Sisi
  • Huduma zetu
  • Uongozi
  • Wasiliana Nasi

Msaada

  • Sera ya Faragha
  • Vigezo & Masharti
  • Msaada
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Usaidizi

Wasiliana Nasi

  • Madaraka Avenue, Kivukoni, Tanzania
  • info@hazinasaccos.co.tz
  • +255 710 933 944

© 2025 Hazina SACCOS. Haki zote zimehifadhiwa.