info@hazinasaccos.co.tz +255 710 933 944
English | Swahili
Contact Us
emblem

HAZINA SACCOS

HAZINA SAVING AND CREDIT COOPERATIVE SOCIETY LTD
CHAMA CHA USHIRIKA WA AKIBA NA MIKOPO CHA HAZINA
hazina Logo
  • Kuhusu Sisi
    Historia Dira, Dhamira & Maadili Ukuaji
  • Uongozi
    Muundo Wajumbe wa Board Menegementi Kamati Ya Usimamizi Watendaji
  • Huduma Zetu
    Akiba Hisa Amana Mikopo Historia
  • Habari & Matukio
    Habari Matukio Video Maswali ya Wateja
  • Mifumo
    Portal Yetu Staff Mail
  • Nakala
  • Wasiliana Nasi
  1. Akiba
 1. Utangulizi

Akiba ni fedha anazochangia mwanachama ili kuwa na sifa ya kupata huduma za mikopo. Fedha hii hairuhusiwi kutoka ama kupungua mara kwa mara isipokuwa kama ilivyoelekezwa katika Masharti ya Chama

2. Aina Za Akiba

Hazina Saccos Limited SACCOS Ltd itakuwa na makundi makuu 2 ya Akiba

    (a)   Akiba Za Lazima
    (b)   Akiba Za Hiyari

Akiba ya lazima inamfanya mwanachama kuwa na sifa ya kupata huduma ya mikopo na akiba hii haitachezacheza kwa maana ya kutoka ama kupungua kama inavyoelekezwa kwenye Masharti ya Chama


Akiba ya hiyari ni akiba anayojiwekea mwanachama kwa malengo mahsusi na akiba hii inaweza kutolewa ama kupunguzwa muda wowote. Endapo kiwango kinachotolewa ama kupunguzwa ni kikubwa kuliko kiwango kilichowekwa katika Masharti basi Mwanachama atatakiwa kutoa notisi ya siku 14.

3. Aina ya Mazao ya Akiba ya Hiyari

Mwanachama anaweza kuweka akiba yake ya hiyari katika moja ya mazao yafuatayo:-

-Akiba Ya Malengo Maalum

   (a)  Akiba Ya Watoto
   (b)  Akiba Ya Elimu
   (c)   Akiba Ya Sikukuu
   (d)  Akiba Ya Wasitaafu
   (e)  Akiba Ya Jamii
   (f) Akiba Ya Mshahara


4. Riba Juu Ya Akiba

Kila mwaka Hazina Saccos Limited kupitia Mkutano Mkuu itaweka kiwango cha riba juu ya akiba za wanachama ili kuwezesha ongezeko la thamanai ya akiba hizo. Kwakuwa hii ni gharama ya kifedha kwenye Chama itakuwa inabadilika kila mwaka kutokana na mwelekeo wa makisio ya mapato na matumizi.

Mwanachama akikoma kuwa mwanachama wa Hazina SACCOS Ltd atatakiwa kuandika notisi na akiba zake atarejeshewa baada ya siku 90 tokea kupokelewa na notisi hiyo.



Hazina Saccos

Chama cha ushirika wa akiba na mikopo kilichopo Tanzania, kinachotoa huduma za kifedha kwa wanachama wake ili kuwasaidia kujiimarisha kiuchumi.

Viungo Muhimu

  • Kuhusu Sisi
  • Huduma zetu
  • Uongozi
  • Wasiliana Nasi

Msaada

  • Sera ya Faragha
  • Vigezo & Masharti
  • Msaada
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Usaidizi

Wasiliana Nasi

  • Madaraka Avenue, Kivukoni, Tanzania
  • info@hazinasaccos.co.tz
  • +255 710 933 944

© 2025 Hazina SACCOS. Haki zote zimehifadhiwa.