- Maana Ya Hisa
Sheria ya Ushirika na. 6 ya mwaka 2013 kupitia kifungu cha 41 inatambua uwepo wa Mwanachama (member) na Mteja (client), ikiwa mwanachama ni yule aliyenunua hisa ndani ya chama wakati mteja ni yule anayetumia huduma za akiba na amana ndani ya Chama. Hisa ni uwekezaji wa msingi kabisa kwa Mwanachama. Hisa humfanya mwanachama kuwa mmilikia halali wa SACCOS.
2. Aina Za Hisa
Kuna aina mbili za hisa ambazo mwanachama anaweza kuchangia ambazo ni;
2. Aina Za Hisa
Kuna aina mbili za hisa ambazo mwanachama anaweza kuchangia ambazo ni;
(a) Hisa Za Lazima
(b) Hisa Za Ziada
(b) Hisa Za Ziada
Hisa za lazima ndiyo hisa za umiliki wa Chama, ni kiwango cha chini cha hisa ambazo kila mwanachama anatakiwa kumiliki ndani ya Chama. Hadi sasa hisa za msingi kwa HAZINA SACCOS Ltd ni kama ifuatavyo;
(a) Kiwango Cha Chini Cha Idadi Ya Hisa ni 25
(b) Thamani Ya Kila Hisa Ni Tsh 20, 000/=
(c) Hivyo Kiwango Cha Chini Cha Thamani Ya Hisa Kwa Kila Mwanachama Ni Tsh 500, 000/=
(a) Kiwango Cha Chini Cha Idadi Ya Hisa ni 25
(b) Thamani Ya Kila Hisa Ni Tsh 20, 000/=
(c) Hivyo Kiwango Cha Chini Cha Thamani Ya Hisa Kwa Kila Mwanachama Ni Tsh 500, 000/=
Hisa za ziada ni zile ambazo mwanachama atachangia juu ya hisa za msingi. Aidha mwanachama anaweza kuchangia hisa za ziada mpaka 20% ya Hisa zote za Chama(Hazina Saccos Limited).